Habari Za Un

Informações:

Sinopsis

Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Episodios

  • 22 MEI 2024

    22/05/2024 Duración: 10min

    Hii leo jaridani tunaangazia huduma za afya kwa watoto nchini Haiti na simulizi afisa wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni WHO kuhusu yanayoenndelea Gaza. Makala tnakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Tanzania, kulikoni? Ghasia zikiwa zinaongezeka katika mji mkuu wa Haiti, Port-Au-Prince, hospitali sita kati ya kumi nchini humo ziko katika hali mbaya ya utoaji huduma limeonya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF. Afisa wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni WHO aliyerejea hivi karibuni kutoka Ukanda wa Gaza amesimulia yale aliyoshuhudia akiwa huko huku huku akisisitiza kuwa "hakuna mahali salama" katika Ukanda huo na aliyoshuhudia ni “yakusitikisha na ya kutisha.”Makala inatupeleka Kaunti ya Garisa nchini Kenya ambako waathirika wa mafuriko na maporomoko ya udongo ya hivi karibuni walio katika makambi za muda za wakimbizi wa ndani wanapokea msaada wa fecha na vocha kutoka kwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wake ikiwa

  • Niliyoshuhudia Gaza yanatisha na kusikitisha - Nika Alexander

    22/05/2024 Duración: 02min

    Afisa wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni WHO aliyerejea hivi karibuni kutoka Ukanda wa Gaza amesimulia yale aliyoshuhudia akiwa huko huku huku akisisitiza kuwa "hakuna mahali salama" katika Ukanda huo na aliyoshuhudia ni “yakusitikisha na ya kutisha.”Ni Nika Alexander kiongozi wa timu ya mawasiliano ya dharura kutoka WHO akieleza tofauti ya kwanza anayoona sasa akiwa amerejea kutoka Gaza ambapo wakati angali kule siku baada ya siku wakisikia mlio wa ndege basi bomu linaweza kuanguka dakika yoyote, wakati sasa ukiwa sehemu ambayo si ya vita akisikia mlio wa ndege pengine ni watu wanaendea likizo ni kama watu wa Gaza wanaishi kinyume na ulimwengu. Akihojiwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa baada ya kurejea Gaza Bi.Nika anasimulia hali ya kule. “Nilichoondoka nacho ni mawazo ya jinsi hali ilivyo mbaya kwa watu wa Gaza, jinsi hali ilivyo ngumu kwa watu wanaojaribu kuwasaidia watu wa Gaza na jinsi kulivyo hatari.” Amesema hospitali zinazofanya kazi ni chache na hazifanyi kazi kamili.“Kim

  • 21 MEI 2024

    21/05/2024 Duración: 10min

    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kufuatilia mradi wa mradi wa Cookfund, Elisabeth Ngoye amezungumza na Laurien Kiiza wa UNIC Dar es Salaam. Pia tunakuletea muhtasari wa habari zikiwemo za afya, Gaza na Ukraine. Mashinani inatupeleka nchini Kenya, kulikoni? Ripoti mpya iliyotolewa leo Mei 21 na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO inaashiria ongezeko kubwa la magonjwa ya zinaa duniani, huku kukiwa bado na changamoto za Virusi Vya Ukimwi na homa ya ini. Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X ameeleza wasiwasi mkubwa walio nao juu ya usalama wa wagonjwa na wafanyakazi waliokwama katika hospitali ya Al-Awda kaskazini mwa Gaza.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) nchini Ukraine, limeeleza kuhusu wasiwasi mkubwa kutokana na hali inayozidi kuwa mbaya na kusababisha ongezeko la mahitaji ya kibinadamu kwa Waukraine na kulazimishwa kuyahama makazi yao kutokana na mashambulizi mapya ya ardhin

  • Ninajisikia fahari sana kutatua changamoto za wanawake na watoto wa CAR - Meja Lilian Laizer

    20/05/2024 Duración: 03min

    Makala hii inamwangazia Meja Lilian Laizer, Mlinda amani wa Umoja wa Mataifa anayehudumu katika Kikosi cha 7 cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania TANBAT 7 kinachohudumu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR chini ya MINUSCA ambao ni Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani nchini humo. Meja Lilian Laizer anashughulika na masuala ya jinsia na watoto katika kikosi na jamii ya wenyeji. Msimulizi ni Anold Kayanda

  • Baadhi ya wapalestina warejea kwenye nyumba zao zilizoathiriwa na mabomu baada ya kulazimishwa kuondoka Rafah

    20/05/2024 Duración: 02min

    Kuongezeka kwa shughuli za kijeshi huko Rafah, kusini mwa Gaza, kumesababisha mamia kwa maelfu ya watu kuyahama makazi yao, na kufanya maisha kuwa magumu zaidi kwa maelfu ya familia ambazo tayari zimelazimika kuyahama makazi yao mara kadhaa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani WFP lina wasiwasi mkubwa kwamba hali hii ya kuhama hama inaweza kusababisha janga la kibinadamu, nakupelekea kusimama kwa shughuli za kutoa misaada ya kibinadamu.Baada ya kufika nyumbani kwake, Ibrahim Kamal Ibrahim Amtair anamuonesha mtoto wake mdogo wa kike box lililojaa bidhaa mbalimbali za msaada aliopokea kutoka WFP. Ibrahim ni mmoja wa watu waliokimbia makazi yao Khan Younis na kukimbilia Rafah baada ya amri ya Jeshi la Israel lakini baada ya Israel wiki iliyopita kutoa tena amri ya kuwataka kuondoka Rafah ameona hana tena pa kukimbilia na kuamua kurejea katika nyumba yake. Amekuta nyumba yake imeathirika vibaya na mabomu pamoja na risasi, baadhi ya maeneo hakuna madirisha wala milango huku kukiwa na

  • 20 MEI 2024

    20/05/2024 Duración: 11min

    Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya sheria na uhalifu na hali ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza. Makala tunakupeleka nchini CAR kufatilia kazi za walinda amani na mashinani tunakuletea ukumbe kuhusu ufugaji nyuki na thamana yao. Mwendesha Mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC, Karim Khan ametangaza leo Mei 20 maombi ya hati za kukamatwa viongozi wa Hamas na Israel kwa madai ya kuhusika na uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu katika eneo la Gaza. Kuongezeka kwa shughuli za kijeshi huko Rafah, kusini mwa Gaza, kumesababisha mamia kwa maelfu ya watu kuyahama makazi yao, na kufanya maisha kuwa magumu zaidi kwa maelfu ya familia ambazo tayari zimelazimika kuyahama makazi yao mara kadhaa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani WFP lina wasiwasi mkubwa kwamba hali hii ya kuhama hama inaweza kusababisha janga la kibinadamu, nakupelekea kusimama kwa shughuli za kutoa misaada ya kibinadamu.Makala inamwangazia Meja Lilian Laizer, Mlinda amani wa Umoja wa Mataifa

  • ICC yawasilisha ombi kwa Baraza la Usalama la hati za kukamatwa viongozi wa Hamas na Netanyahu wa Israel

    20/05/2024 Duración: 02min

    Mwendesha Mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC, Karim Khan ametangaza leo Mei 20 maombi ya hati za kukamatwa viongozi wa Hamas na Israel kwa madai ya kuhusika na uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu katika eneo la Gaza. Ni Karim Khan, Mwendesha Mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu mapema leo alipotangaza kwamba anawasilisha maombi ya hati za kukamatwa viongozi wa Hamas na wa Israel kwa majaji wa mahakama hiyo ambao ndio watakaotoa uamuzi wa kutolewa kibali cha kukamatwa.Bwana Khan amesema kuna sababu za msingi za kuamini kwamba Yahya Sinwar wa Hamas, Mohammed Diab Ibrahim Al-Masri (Deif) na Ismail Haniyeh "wanawajibikia kijinai" kwa mauaji, kuangamiza na kuchukua watu mateka miongoni mwa uhalifu mwingine mwingi tangu mzozo wa Gaza ulipozuka kufuatia mashambulizi yaliyoongozwa na Hamas kusini mwa Israel tarehe 7 Oktoba mwaka jana 2023.“Pia kuna misingi ya kuridhisha ya kuamini kwamba Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na Yoav Gallant, Waziri wa Ulinzi wa I

  • Orodha mpya ya bakteria sugu dhidi ya dawa yatolewa na WHO

    17/05/2024 Duración: 01min

    Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo limetoa Orodha mpya ya inayojumuisha familia 15 za bakteria zenye usugu dhidi ya viuavijiumbe maradhi au antibiotics. Orodha hiyo inatoa mwongozo kuhusu maendeleo ya matibabu mapya na ya lazima ili kukomesha kuenea kwa usugu dhidi ya dawa. Katika taarifa iliyotolewa leo, WHO inafafanua kuwa usugu wa vijiumbemaradhi dhidi ya dawa hutokea pale ambapo bakteria, virusi, fangasi, na vimelea vingine vya magonjwa haviitikii tena dawa, hivyo kuongeza hatari ya kusambaa kwa magonjwa, watu kuugua na hata vifo.WHO inaeleza kwamba kwa sehemu kubwa hali hii ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa inasababishwa na matumizi mabaya ya dawa za viuavijumbe maradhi.Utafiti huu mpya uliotolewa leo unajumuisha uthibitisho mpya na maarifa ya kitaalamu ili kuongoza utafiti na maendeleo kwa ajili ya viuavijiumbemardahi yaani Antibiotics mpya na kuhamasisha uratibu wa kimataifa ili kukuza uvumbuzi.Baadhi ya bakteria sugu zilizotajwa ni Neisseria gonorrhoeae i

  • Uchumi wa dunia umeboreka kidogo ingawa Afrika bado kuna changamoto - Nelly Muriuki

    17/05/2024 Duración: 06min

    Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya katikati ya mwaka ya hali na mtazamo wa uchumi wa Dunia kwa mwaka 2024 iliyotolewa leo inaonyesha matarajio ya kiuchumi duniani yameboreka tangu utabiri uliotolewa Januari 2024, lakini mtazamo ni wa matumaini yanayohitaji tahadhari. Je, Afrika hali iko vipi? Flora Nducha amezungumza na Nelly Rita Muriuki mchumi kutoka Idara ya masuala ya kiuchumi na kijamii ya Umoja wa Mataifa DESA ambao ndio wamezindua ripoti hiyo. 

  • 17 MEI 2024

    17/05/2024 Duración: 10min

    Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya usugu dhidi ya viuavijiumbe maradhi au antibiotics, na hali ya kibinadamu nchini Ukraine. Makala tunasalia hapa hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa na mashinani tunaelekea nchini Afghanistan, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo limetoa Orodha mpya ya inayojumuisha familia 15 za bakteria zenye usugu dhidi ya viuavijiumbe maradhi au antibiotics. Orodha hiyo inatoa mwongozo kuhusu maendeleo ya matibabu mapya na ya lazima ili kukomesha kuenea kwa usugu dhidi ya dawa. Mashirika ya kibinadamu yanafanya kazi bila kuchoka kusaidia kuwaondoka raia katika eneo la Kharkiv ambalo siku za hivi karibuni limeshuhudia kuzorota kwa hali ya usalama na kutanda kwa wimbi la mapigano ambayo yamesababisha vifo vya raia na majeruhi ikiwa ni pamoja na watoto.Makala inaturejesha hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa kulikozinduliwa ripoti ya nusu mwaka ya mtazamo wa ukuaji na matarajio ya uchumi wa Dunia kwa mwaka 2024. Je Afrika hali iko vipi? Flora Nducha amezun

  • Mashirika ya kibinadamu yanahaha kuondoa watu huko Kharkiv Ukraine

    17/05/2024 Duración: 02min

    Mashirika ya kibinadamu yanafanya kazi bila kuchoka kusaidia kuwaondoka raia katika eneo la Kharkiv ambalo siku za hivi karibuni limeshuhudia kuzorota kwa hali ya usalama na kutanda kwa wimbi la mapigano ambayo yamesababisha vifo vya raia na majeruhi ikiwa ni pamoja na watoto. Video ya ofisi kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura ya Umoja wa Mataifa, OCHAinaanza kwa kuonesha watu wakishuka katika bus, hawa ni raia walioondolewa huko Kharkiv ambako mapigano kati ya Ukraine na Urusi yanaendelea. Uokoaji unaendelea kupitia mabasi yanayoratibiwa na mashirika ya misaada ya kibinadamu, watu binafsi wanaojitolea na serikali za mitaa. Kwa mujibu wa OCHA kati ya tarehe 10 na 15 Mei, karibu watu 2,400 wamefanikiwa kuhamishwa na kuletwa kwenye kituo cha muda ambapo wanapokea usaidizi. Mmoja wa watu hao ni Bibi huyu aitwaye Valentyna anayetujuza hali ilivyokuwa huko alipotoka "Sisi kwetu ni Okhrimivka. Tunaishi pamoja na binti yangu ambaye ni mlemavu.  Kijiji chetu kilipigwa na

  • Jifunze Kiswahili: Pata uchambuzi wa neno “HIZAYA.”

    16/05/2024 Duración: 50s

    Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “HIZAYA.” 

  • 16 MEI 2024

    16/05/2024 Duración: 11min

    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Bahrain kwenye mji mkuu Manama, ambako wajasiriamali wamekusanyika kwa lengo la kutumia ugunduzi na ujasirimali kusongesha SDGs. Pia tunakuletea muhtasariwa habari kutoka ICJ, WHO na huko huko Bahrain, pamoja na uchambuzi wa neno “HIZAYA.”Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amerejea wito wake wa kutaka usitishwaji wa mashambulizi huko Rafah kwani wananchi wanazidi kuteseka kutokana na kulazimika kuhama kila wakati huku wakikosa huduma muhimu za kijamii ikiwemo msaada wa chakula na matibabu. Hii leo Mahakama ya Haki ICJ inasikiliza ombi kutoka taifa la Afrika Kusini ambalo linaiomba mahakama hiyo kuliwekea vikwazo zaidi jeshi la Israel ambalo linafanya mashambulizi ya anga na ardhini huko Ukanda wa Gaza mashambulizi ambayo yamegharibu maelfu ya maisha ya watu.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO hii leo limetoa muhtasari wa ugonjwa wa kipindupindu ulimwenguni ambao mpaka sasa umetajwa kuenea katika mataifa 24 katik

  • Mafunzo ya UNIDO yameboresha bidhaa zetu sasa tunahitaji masoko ya uhakika

    15/05/2024 Duración: 03min

    Huko Manama mji mkuu wa Bahrain huko Asia ya Magharibi kunafanyika mkutano wa tano wa Jukwaa la Uwekezaji kwa wajasiriamali, WEIF 2024. Zaidi ya washiriki 1000 ni wajasiriamali kutoka Afrika wakisaka kujenga mitandao na ubia ili kusaka masoko ya uhakika ya bidhaa zao na hatimaye kuondokana na umaskini, moja ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs ya Umoja wa Mataifa. Mkutano umeandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la maendeleo ya Viwanda, UNIDO ofisi ya ugunduzi wa teknolojia, ITPO nchini Bahrain. Assumpta Massoi aliyeko Manama anazungumza na mjasiriamali kutoka Kenya, Edith Lewela, Mwenyekiti wa kundi la wanawake wajasiriamali wa Taita-Taveta na pia mnufaika wa mafunzo ya ujasiriamali yaliyotolewa na UNIDO mwaka 2009. Bi. Lewela anaanza kuelezea manufaa ya mafunzo hayo ambayo anapatia pia wenzake.

  • Ziara za Catriona Laing za kuwaaga viongozi Somaliland

    15/05/2024 Duración: 01min

    Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Catriona Laing ameendelea na ziara yake ya kuwaaga viongozi wa eneo hilo na sasa ametembelea Somaliland. Juzi Mei 12, Catriona Laing alikuwa  Dusmareb, mji mkuu wa jimbo la Galmudug katikati mwa Somalia ambako alipongeza juhudi za kupambana na ukeketaji. Kisha jana Mei 14 akatua Hargeisa mji mkuu wa Somaliland ambako  amekutana na uongozi na kujadili msaada wa Umoja wa Mataifa kwa maendeleo na juhudi za kibinadamu. Miongoni mwa aliokutana nao ni Rais Muse Bihi na wajumbe wa baraza lake la mawaziri na washauri."Tumekuwa na mjadala mzuri sana, na Rais amezungumza nami kuhusu mpango wa maendeleo, ambao unaweka maono yake ya muda mrefu ya kiuchumi kuhusu faida za 'uchumi wa buluu,' kuhusu madini, na kufikiria juu ya mabadiliko ya biashara ya mifugo kama tunajiandaa dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi kwa watu wenye maisha ya kuhamahama. Tumezungumza kuhusu jukumu la Umoja wa Mataifa katika kuunga mkono kufanikisha dira ya ki

  • 15 MEI 2024

    15/05/2024 Duración: 10min

    Hii leo jaridani tunaangazia machafuko Gaza, na ziara za Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Catriona Laing. Makala tunakupeleka mjini Manama huko Bahrain na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yameendelea kuonya kuhusu hali mbayá ya Rafah Gaza ambako mashambulizi ya Israel yanaendelea kukatili Maisha ya watu na kulazimisha maelfu kufungasha vitago tena kwenda kusaka usalama. Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Catriona Laing ameendelea na ziara yake ya kuwaaga viongozi wa eneo hilo na sasa ametembelea Somaliland.Makala tunakwenda Manama mji mkuu wa Bahrain huko Asia ya Magharibi kunakofanyika mkutano wa tano wa Jukwaa la Uwekezaji kwa wajasiriamali, WEIF 2024 ambapo Assumpta Massoi amezungumza na mjasiriamali kutoka Kenya, Edith Lewela, Mwenyekiti wa kundi la wanawake wajasiriamali wa Taita-Taveta. Yeye ni mnufaika wa  mafunzo ya ujasiriamali yaliyotolewa na UNIDO mwaka 2009, sasa anafundish

  • UN: Hali Rafah ni mbayá mashambulizi yanakatili maisha na kufurusha watu kwa maelfu

    15/05/2024 Duración: 01min

    Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yameendelea kuonya kuhusu hali mbayá ya Rafah Gaza ambako mashambulizi ya Israel yanaendelea kukatili maisha ya watu na kulazimisha maelfu kufungasha vitago tena kwenda kusaka usalama. Kwa mujibu wa tarifa ya shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA kuendelea kwa mashambulizi ya wanajeshi wa Israel, kwenye Ukanda wa Gaza kwa njia ya angani, ardhini na baharini kunazidisha vifo vya raia, kulazimika wengi kukimbia na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya makazi na miundombinu mingine muhimu ya raia. Shirika hilo limeongeza kuwa na mashambulizi ya ardhini ya Israeli yanaendelea kupanua wigo, haswa katika maeneo ya kusini mwa mji wa Gaza na Mashariki mwa Rafah, hususan karibu na Kerem Shalom na vivuko vya Rafah.Kana kwamba hayo hayatoshi Philippe Lazzarini ambaye ni Kamishina Mkuu wa UNRWA amesema kumekuwa na jaribio lingine la uchomaji moto la watoto na vijana wa Israel kwenye majengo ya UNRWA huko Jerusalem jana usiku. A

  • 14 MEI 2024

    14/05/2024 Duración: 11min

    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inamulika ugunduzi na ukuaji uchumi. Shirika la Umoja wa Mataifa la maendeleo ya viwanda, UNIDO ni sehemu ya wawezeshaji wa jukwaa la WEIF 2024 na mwakilishi wake amezungumza na mwenyeji wetu huko Manama Bahrain Assumpta Massoi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani.Huko Gaza Wapalestina zaidi waliouawa kutokana na mashambulizi ya kijeshi ya Israel wakiendelea kutambuliwa na mamlaka ya afya ya eneo hilo, wasaidizi wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wameeleza tena kwamba kwa hakika katika ya watu 35 ambao wameshauawa, idadi kubwa ya wanawake na watoto. Kufuatia tathmini za kina nchini Malawi na Msumbiji, Timu huru ya Tathmini ya Kukabiliana na Mlipuko wa Polio (OBRA) leo Mei 14 imependekeza kufikia ukomo wa mlipuko wa virusi vya polio aina ya 1 (WPV1) nchini Malawi na Msumbiji, kuashiria hatua muhimu katika mapambano dhidi ya polio katika eneo la Afrika. Kisa cha mwisho cha WPV1 katika Kanda ya Afrika, kilichohusishwa na aina hiyo ya polio kiliri

  • Uwekezaji kwa wajasiriamali duniani kumulikwa Manama, Bahrain

    13/05/2024 Duración: 04min

    Jukwaa la 5 la kimataifa la uwekezaji kwa wajasiriamali, WEIF 2024 linaanza kesho kwenye mji mkuu wa Bahrain, Manama ukileta pamoja washiriki zaidi ya 1000, wakiwemo wajasiriamali kutoka pembe zote za dunia. Jukwaa hili linafanyika kwa siku tatu na na maudhui ni kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kwa kuendeleza uvumbuzi na ukuaji wa kiuchumi. Jukwaa hili linalenga basi kupatia majawabu changamoto za dunia ikiwemo umaskini, ukosefu wa usawa, mabadiliko ya tabianchi, amani, haki kwa muktadha wa SDGs. Dkt. Hashim Hussein, ni mtaalamu wa kuendeleza uwekezaji katika shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda, UNIDO anaeleza ni nini hasa wanatarajia kutoka jukwaa hili alipopata fursa kuzungumza na Assumpta ambaye tayari yuko Manama kutujuza kitakachojiri.

  • Mashirika ya UN yaonya kuwa maelfu ya maisha ya watu El Fasher Sudan yako hatarini

    13/05/2024 Duración: 01min

    Mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa leo yameonya kwamba maisha ya maelfu ya watu yako hatarini El Fasher Sudan, kufuatia mashambulizi makali yanayoendelea ambapo moja ya hospitali Darfur Kaskazini imeshambuliwa na kukatili maisha ya watu wawili lakini pia kuchochea hofu ya kurejea kwa baa la njaa. Kwa mujibu wa Mratibu wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths, “Shambulio hilo limeharibu paa la hospitali katika kituo cha huduma za dharura kwenye Hospitali ya Sourthen katika mji wa El Fasher ambayo ndio hospitali pekee inayofanyakazi kwas asa katika jimbo la Darfur Kaskazini na ambako vifaa vya matibabu na dawa sasa karibu vinakwisha.” Amesema takriban watu 800,000 wanaishi katika mji wa El Fasher na maelfu ya maisha yao yako hatarini huku taifa zima la Sudan likiwa katika hali mbaya.Shirika la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA limesema makumi ya raia waliuawa mwishoni mwa wiki katika mapigano mapya  makubwa yaliyozuka Ijumaa kati ya vikosi vya se

página 2 de 5