Gurudumu La Uchumi

Fursa za uwekezaji nchini Bostwana kwa nchi za Afrika Mashariki

Informações:

Sinopsis

Kati ya Oktoba 11 hadi 14 mwezi Oktoba, Bostwana iliandaa maonesho ya Kimataifa ya kibiashara jijini Gaborone, yaliyofanyika pembezoni mwa Jukwaa la kwanza wa kibiashara kati ya nchi hiyo na Umoja wa Ulaya. Bostwana ambayo uchumi wake mkubwa unategemea sekta ya madini, hasa Almasi ikiwa ya pili duniani kwa bidhaa hiyo baada ya Urusi, ilitumia fursa hiyo kujitangaza na kuvutia wawekezaji zaidi.Nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika ambayo inataka kuwa nchi ya kipato cha juu kufikia 2036 kwa kupanua uchumi wake kwenye sekta nyingine kama kilimo na utalii, ni miongoni mwa mataifa duniani, ambayo taasisi za Kimataifa kama IMF na Benki ya dunia, zinasema uchumi wake unakuwa kwa kasi.Je, Bostwana ina fursa zipi za uwekezaji hasa kwa mataifa ya Afrika Mashariki ? Wakati wa maonesho hayo, nilitembelea banda la Kenya, na leo kwenye Makala yetu ya Gurudumu la Uchumi, utamsikia Balozi wa Kenya nchini Bostwana.