Gurudumu La Uchumi

Viongozi wa dunia wajadili malengo endelevu ya umoja wa Mataifa

Informações:

Sinopsis

Mwezi uliopita, viongozi wa dunia walikutana jijini New York, Marekani katika mkutano wa 78 wa baraza la umoja wa Mataifa, ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ikiwemo usalama wa dunia na ukuaji wa uchumi pamoja na mikakati ya kufikia ajenda ya mwaka 2030 na haja ya kuongeza kasi kutekeleza malengo 17 endelevu. Kuzungumzia yaliyojiri, mtayarishaji wa makala haya alimualika Ebenezer Suleiman Mathew Ikomba, balozi wa vijana wa Tanzania kwenye umoja wa Mataifa. Katika mijadala mingi, vijana walitajwa kuwa sehemu kubwa ya nguvu kazi ya dunia na kwamba kupitia ubunifu, uwajibikaji na harakati za kuhamasisha nchi kufikia malengo endelevu, basi dunia itakuwa sehemu salama. Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili inaangazia yaliyotokana kwenye mkutano huo na namna gani vijana wanaweza kushiriki katika ujenzi wa dunia salama na yenye amani ambayo itachochea maendeleo na ukuaji wa uchumi.