Gurudumu La Uchumi

IMF, benki ya dunia zaonya kuhusu kudorora kwa uchumi wa mataifa ya Afrika

Informações:

Sinopsis

Ukuaji wa uchumi wa nchi za Afrika zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara, unatarajiwa kupungua kasi mwaka huu, kutokana na kudorora kwa uchumi wa mataifa ya Afrika Kusini, Nigeria na Angola, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya Dunia.Ukuaji wa kikanda utapungua hadi 2.5% mwaka 2023 kutoka 3.6% mwaka jana, imesema ripoti hiyo.Mtayarishaji amezungumza na Johnson Denge, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi, kuangazia ripoti hizi kwa kina. Aidha kwa mujibu wa IMF Uchumi wa dunia unakua lakini sio kwa kasi, ambapo inakadiria kuwa ukuaji wa uchumi wa dunia utapungua kutoka asilimia 3.5 mwaka 2022 hadi asilimia 3 mwaka huu na asilimia 2.9 mwaka ujao. IMF inasema Mfumuko wa bei ambao haujumuishi bei ya chakula na nishati pia unatarajiwa kupungua, ingawa polepole zaidi. Nchi nyingi zikitajwa kutokuwa na uwezekano wa kurudisha mfumuko wa bei hadi 2025.